To Advertise on this Blog please Call: O713 397 767 or 0785 555 560                                                 To Advertise on this Blog please Call: O713 397 767 or 0785 555 560
Mail Me

Friday, October 7, 2011

Baba Ashikiliwa Na Jeshi La Polisi Mkoani Mbeya Kwa Kosa La Kumshinikiza Mkewe Kunywa Sumu Hadi Kufa

Mtuhumiwa Bwana Mohamed Mwawipa ambaye alimshinikiza mkewe Nuru Masuba kunywa sumu baada ya kumtuhumu kuwa amemwibia fedha taslimu shilingi laki nne na elfu hamsini akionesha askari wa upelelezi eneo alilonywea sumu mkewe

Mwili wa marehemu Nuru Masuba aliyeshinikizwa kunywa sumu baada ya kutuhumiwa kumwibia fedha shilingi laki nne na elfu hamsini na Mumewe Mohamed Mwawipa akipelekwa kuhifadhiwa kaburini, baada ya uchunguzi wa daktari na polisi kukamilika.

Mweyekiti wa kijiji cha Ijumbi kata ya Ruiwa wilaya ya Mbrali Bwana John Mkalimoyo akimfariji dada wa marehemu Nuru Masuba aitwaye Stumai Wilson ambapo marehemu alikuwa akiishi naye Kijiji cha Mapogolo kapunga.
 
Mohamed Mwawipa mwenye umri wa miaka 50 mkazi wa kijiji cha Ijumbi kata ya Luwiwa wilayani Mbarali mkoani Mbeya ameshikiliwa na jeshi la Polisi wilayani humo kwa tuhuma za kumshinikiza mke wake kunywa sumu baada ya kumtuhumu kumwibia shilingi laki nne na elfu hamsini.
Habari kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa marehemu Nuru Masuba alikuwa na ugomvi kwa kipindi kirefu na mumewe hali aliyopelekea wakatengana, lakini oktoba 4 walirejeana upya mahusiano yao mpaka kifo kilipomfika.
Akiongelea tukio hilo mwenyekiti wa kijiji cha Ijumbi John kalikumoyo amesema mtuhumiwa alikiri kutenda tukio hilo baada kuhojiwa na uongozi wa kijiji na kwamba endapo mwanamke huyo asingekubali kunywa sumu angetumia silaha ya jadi aina ya kisu kumuangamiza kama fedha aizo hazitoonekana.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi alipoulizwa juu ya kukamatw kwa Mohamedi Mwawipa alisema kuwa taarifa hizo bado hazijamfikia na kwamba atazitolea taarifa pindi atakapo pat taarifa kamilikutoka kwa mkuu wa polisi wilaya ya Mbarali.

No comments: