To Advertise on this Blog please Call: O713 397 767 or 0785 555 560                                                 To Advertise on this Blog please Call: O713 397 767 or 0785 555 560
Mail Me

Monday, November 14, 2011

Kufuga Samaki Na Kilimo Cha Mpunga Kwa Pamoja

Naibu Katibu Mkuu Wizara Kilimo Chakula na Ushirika Mhandisi Mbogo Futakamba akifungua mkutano wa unajadili uboreshaji wa mazao ya uvuvi na mpunga kwa ukanda wa Afrika Mashariki jana (leo) jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa siku tano unalenga kuwawawezesha wakulima kuzalisha mpunga kwa wingi huko wakiendeleza ufugaji wa samaki katika maeneo yao ya kilimo ili kupunguza umaskini.
Picha na Tiganya Vincent- MAELEZO- Dar es salaam.


Na Glady Sigera- MAELEZO- Dar es salaam

Wadau wa kilimo na uvuvi nchini wametakiwa kutumia maji yaliyopo kwa ufanisi ili waweze kupata mazao mengi kwa ajili ya kuwasaidia kupata mazao mengi kwa mahitaji ya Tanzania na nje nchini.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo , Chakula na Ushirika Mhandisi Mbogo Futakamba wakati akiongea na waandishi wa Habari mara baada ya kufungua mkutano wa siku tano wa wadau wa kilimo cha mpunga na ufugaji wa samaki kwa Afrika Mashariki.
Alisema kuwa hali ilivyo sasa wakulima wengi wa mpunga hawawezi kutumia vyanzo vyao vya kilimo cha umwagiliaji ipasavyo kama vile kulima mpunga wakati huo huo wanafuga samaki ambao wangweza kuwa saidia kama chakula na kuuza kwa ajili ya kujiongezea kipato na kuondokana na umaskini.
Naibu Katibu Mkuu huyo aliongeza kuwa mkutano huo unaozishirikisha nchi mbalimbali unaandaa mikakati itakayomsaidia mkulima kulima na kufuga samaki kwa wakati mmoja kama sehemu kuongeza uzalishaji nchini wa mazao ya mpunga na uvuvi kwa wakati mmoja.
Alisemakuwa kilimo cha aina ndio kinaweza kuwasaidia wakulima wampunga nchini na wale wa Afrika mashariki kuondokana na upungufu wa chakula na samaki.
Hata hivyo Mhandisi Futakamba alisema kuwa jumla ya bilioni 500 zinahitajika kila mwaka ili kuwezesha kilimo cha hekta laki tano (500,000) za mpunga ili kuhakikisha kunakuwepo na uzalishaji wa kutosha.
Mkutano huo umeandaliwa na Serikali ya Tanzania ,Shirika la Kilimo na Mazao la Umoja wa Mataifa (FAO) na Shirika la Misaada la Japan(JICA) .

No comments: