To Advertise on this Blog please Call: O713 397 767 or 0785 555 560                                                 To Advertise on this Blog please Call: O713 397 767 or 0785 555 560
Mail Me

Thursday, January 12, 2012

KIKAO CHA KAMATI KUU YA CCM CHAFANYIKA ZANZIBAR

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akiwa na Kamatibu wenzake wa NEC, kwenye kikao cha Kamati Kuu ya CCM, Afisi Kuu ya CCM, Kisiwandui mjini Zanzibar. Kushoto ni Katibu wa NEC, Uchumi na fedha Mwigulu Nchemba na kulia ni Katibu wa NEC, Siasa na Ushirikiano wa Kimataifa Januari Makamba.

Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete akiongoza kikao cha Kamati Kuu ya CCM katika ukumbi wa Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui, Zanzibar, leo. Wengine meza kuu Kushoto ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar) Amani Abeid Karume. na aliyesimama ni Katibu Mkuu wa CCM Wilson Mukama na kulia ni makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Pius Msekwa.

Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama akimkaribisha \Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kufungua kikao cha Kamati Kuu ya CCM mjini Zanzibar leo. Wengine meza kuu kushoto ni ni Mjumbe wa kamati Kuu ya CCM, Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Sheni, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar) Amani Abeid Karume na kulia ni Mjumbe wa Kamati Kuu, Rais Mstaafu Ali Hassani Mwinyi na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Pius Msekwa

Mwenyekiti Mstaafu wa CCM, Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, mjumbe wa Kamati Kuu Rais wa zanzibar Dk. Sheni na Makamu |mwenyekiti wa CCM (Zanzibar), Dk. Amani Abeid Karume wakiwa kwenye kikao cha kamati kuu ya CCM mjini Zanzibar jana.

No comments: