To Advertise on this Blog please Call: O713 397 767 or 0785 555 560                                                 To Advertise on this Blog please Call: O713 397 767 or 0785 555 560
Mail Me

Monday, March 19, 2012

KATIBU MKUU SHERIA AKIKAGUA UJENZI WA MAJENGO YA KUDUMU YA LAW SCHOOL DAR JANA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Fanuel Mbonde (aliyevaa tai) akikagua ujenzi unaoendelea wa majengo ya kudumu ya Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST) mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkuu wa LST Dkt. Gerald Ndika na kushoto ni Msimamizi wa Mradi huo Arch. Alloyce Mushi.

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Fanuel Mbonde (aliyevaa tai) akiongea mwishoni mwa wiki jijini Dar e Salaam alipotembelea ujenzi unaoendelea wa majengo ya kudumu ya Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST). Ujenzi unajumuisha maktaba ya kisasa, vyumba vya mihadhara, jengo la utawala na nyumba za watumishi.

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Fanuel Mbonde (aliyevaa tai) akiongea mwishoni mwa wiki ndani ya jengo la Mahakama ya Mafunzo ambalo ni sehemu ya mradi wa ujenzi unaoendelea jijini Dar es Salaam wa majengo ya kudumu ya Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST). Kulia ni Mkuu wa LST Dkt. Gerald Ndika na kushoto ni Msimamizi wa Mradi huo Arch. Alloyce Mushi. Mradi huo una thamani ya Tshs 16/- bilioni.

No comments: