To Advertise on this Blog please Call: O713 397 767 or 0785 555 560                                                 To Advertise on this Blog please Call: O713 397 767 or 0785 555 560
Mail Me

Sunday, October 2, 2011

Matokeo moto Igunga

UPIGAJI kura katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Igunga jana ulimalizika kwa amani na matokeo ya awali wakati tukienda mitamboni yalionesha mchuano mkali kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Ilipofika saa mbili usiku jana, CCM ilikuwa ikiongoza katika kata 9 kati ya 26 za Jimbo la Igunga ikiwa na kura 8,421 dhidi ya kura 6,197 za Chadema.

Kata hizo ni Ntobo, CCM 730, Chadema 302; Nguvu Moja CCM 694, Chadema 284; Nkinga ambako Rais Mstaafu Benjamin Mkapa alifunga mkutano wa kampeni wa CCM Jumamosi, chama hicho kimepata kura 1,479 na Chadema ikipata kura 1,085.

Nyingine ni Itumba CCM 1,079, Chadema 590; Nanga, CCM 897, Chadema 645; Igulubi CCM 925, Chadema 592 wakati katika Kata ya Mwisi anakotoka Mbunge aliyejiuzulu Rostam Aziz, CCM imeanguka kwa kupata kura 926 dhidi ya 992 za Chadema.

Rostam alijiuzulu wadhifa wake huo alioushikilia kwa miaka 17, akidai amefanya hivyo kutokana na siasa uchwara ndani ya chama hicho tawala.

CCM imeanguka pia katika Kata ya Mbutu ambako imepata kura 1,186 dhidi ya 1,426 za Chadema wakati katika Kata ya Kinungu imeongoza CCM kwa kura 505 dhidi ya kura 263 za Chadema.

Aidha, hadi kufikia saa mbili usiku, katika vituo 53 vya Kata ya Igunga Mjini, tayari vituo 22 vilikuwa matokeo yake yako tayari na CCM ilikuwa ikiongoza kwa kura 1,388 dhidi ya kura 1,287 za Chadema. Jimbo zima lina vituo vya kupigia kura 427.

Kutokana na Chadema kuongoza katika baadhi ya vituo vya mjini, vijana na mashabiki wa chama hicho walikuwa wakishangilia na kuandamana kukisifu chama hicho.

Matokeo ya mjini yalionesha kuwa kwenye Kituo cha Shule ya Msingi Igunga, kituo kidogo cha kwanza Chadema ilipata kura 216, CCM
(201) na CUF (3).

Katika Kituo cha Chipukizi, kituo kidogo cha kwanza Chadema ilipata 98, CCM (87) na CUF (7). Kituo kidogo cha pili Chadema 108, CCM 71 na CUF 4.

Kituo cha Tarafani Chadema 88, CCM (61), CUF (6), kituo kidogo cha pili Chadema (73), CCM (71) na CUF (4). Kituo kidogo cha tatu, Chadema (90), CCM (83) na CUF (7).

Katika kituo cha Stoo ya Pamba, kituo kidogo cha kwanza Chadema (69), CCM (81), CUF (2), kituo kidogo cha pili, Chadema (91), CCM (70), CUF (2)., kituo kidogo cha tatu, Chadema (82), CCM (86), CUF (3).

Kituo kidogo cha nne katika kituo cha Stoo ya Pamba, Chadema (72), CCM (76), CUF (2), kituo kidogo cha tano Chadema (84), CCM (79) na CUF (1).

Katika kituo cha Chipukizi, Chadema (98), CCM (84), CUF (7) kituo kidogo cha pili katika kituo hicho, Chadema (106), CCM (71) na CUF (4).

Awali, shughuli ya upigaji kura katika uchaguzi huo wa kujaza nafasi ya Rostam aliyejiuzulu Julai mwaka huu, ilianza na kumalizika kwa utulivu ambapo wakazi wa jimbo hilo walijitokeza kwa wingi katika vituo vya kupiga kura huku kukijitokeza kasoro chache.
Soma zaidi

No comments: