To Advertise on this Blog please Call: O713 397 767 or 0785 555 560                                                 To Advertise on this Blog please Call: O713 397 767 or 0785 555 560
Mail Me

Friday, March 23, 2012

Rais Kikwete afunga Maadhimisho ya wiki ya Maji kitaifa Iringa

 Rais Jakaya Kikwete leo amefunga Maadhimisho ya Wiki ya Maji Kitaifa Mkoani Iringa. Pamoja na kuhutubia katika kilele hicho pia Rais alipata fursa ya kutembelea mabanda mbalimbali ya maonesho ya watoa huduma za maji na wadau mbalimbali wa maji nchini. Pichani ni Rais Kikwete akiwa katika banda la Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) ambao ni wadhamini wakuu wa maadhimisho hayo ya mwaka huu yaliyofanyika uwanja wa Samora Mjini Iringa. Kulia ni Mkurugenzi wa Mahusiano na Mawasiliano wa SBL, Teddy Mapunda na Meneja Uwajibikaji na Miradi Endelevu wa SBL, Nandi Mwiyombela.



Meneja Uwajibikaji na Miradi Endelevu wa Kampuni ya Bia Serengeti (SBL), Nandi  Mwiyombela,akisaliamiana na kumkaribisha Rais Jakaya Kikwete katika banda la Kampuni ya Bia ya  Serengeti lililopo katika viwanja vya Samora mjini Iringa yalipofanyika maonesho ya wiki ya Maji kitaifa.

Rais Jakaya Kikwete akikabidhi cheti cha shukrani kwa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) na Kupokelewa na Mkurugenzi wake wa Mahusiano na Mawasiliano Teddy Mapunda. Pia SBL walipokea Cheti cha ushiriki wa maonesho hayo.

No comments: